Matukio ya Kisiasa | 16.05.2008
Kituo cha Sheria Zanzibar cha laani kukamatwa kwa watu wa Pemba waliowasilisha waraka kwa Umoja wa Mataifa
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC)Visiwani Zanzibar kimelaani hatua ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuwakamata watu waliowasilisha waraka kwa Umoja wa Mataifa wakitaka kisiwa cha Pemba kijitenge na kuwa huru.
Wananchi hao wakaazi wa Pemba waliwasilisha barua katika Umoja wa mataifa wakitaka kujitenga kwa kisiwa hicho kwa kile walichodai kutopewa umuhimu na serikali ya Zanzibar. Ili kupata ufafanuzi wa Kisheria nimezungumza na Profesa Haroub Othman mwanasheria na mwanaharakati katika kituo cha Sheria na haki za Binadamu Visiwani Zanzibar.












