1. main content
  2. main navigation
  3. extra content
  4. head navigation
  5. search
  6. Choose form 30 Languages



 

 | 09.05.2008 | 14:00 UTC

Mji wa Beirut wakosa watu wakati wafuasi wa Hezboullah wakithibiti sehemu ya magharibi ya mji huo.

Beirut.


Rais  wa  Syria  Bashar al-Assad  ameueleza  mzozo wa  kisiasa  nchini  Lebanon  kuwa  ni  suala  la ndani  ya  nchi  hiyo  ambalo  linapaswa  kutatuliwa kupitia  mazungumzo.

Taarifa  ya  Assad , ambayo  imeripotiwa  na  vyombo vya  habari  nchini  humo, inakuja  katika  siku  ya tatu  ya  mapigano  baina  ya upande  wa  upinzani unaongozwa  na  Hezboullah  na  wafuasi  wa serikali.

Wanamgambo  wa  Hezboullah  hivi  sasa wanadhibiti  eneo  kubwa  la  magharibi  ya  Beirut, wakati  uwanja  wa  ndege  umefungwa  pamoja   na bandari  kuu  ya  mji  huo  kutoweza  kufanya  kazi.

kituo  cha  televisheni  kinachounga  mkono  serikali cha  Future News pia  kimeshindwa  kutoa matangazo  yake.

Wakati  huo  huo wizara  ya  mambo  ya  kigeni  ya Italia  imetangaza  kuwa  inajitayarisha  kuwaondoa raia  wake  kutoka  Lebanon. Ghasia  hizo  zimezuka baada  ya  serikali kutangaza  kuwa  mfumo  wa mawasiliano  wa  kijeshi  wa  kundi  la  Hizboullah  ni kinyume  na  sheria.  Kiongozi  wa   Hezboullah Hassan  Nasrallah  amesema   kuwa  uamuzi  huo wa  serikali  unamaanisha  kutangaza  vita.

Ujerumani  imetoa  wito  leo  wa  kumalizwa  mara moja   kwa  hali  ya  kukosekana  kiongozi  nchini Lebanon , na  kusema  kuwa  hali  hiyo  inazidisha wasi  wasi  ambayo  inaisukuma  nchi  hiyo  katika ukingo  wa  vita  vya  wenyewe  kwa  wenyewe.

Waziri  wa  mambo  ya  kigeni  wa  Ujerumani Frank Walter Steinmeier  amesema  baada  ya kuzungumza  kwa  simu  na  waziri  mkuu  wa Lebanon Fouad  Siniora  kuwa  ana wasi  wasi mkubwa  kuhusiana  na  mapigano  hayo  kati  ya Wasunni  wanaounga  mkono  serikali inayoungwa mkono  na  mataifa  ya  magharibi  na  wapiganaji wa  Kishia.