1. main content
  2. main navigation
  3. extra content
  4. head navigation
  5. search
  6. Choose form 30 Languages



 

News | 09.05.2008 | 14:00 UTC

Utawala wa kijeshi wa Burma waendelea kukataa misaada ya nje.

Rangoon.


Licha  ya  mbinyo  mkubwa  wa  kimataifa  dhidi  ya utawala  wa  kijeshi  wa  Burma  kukubali  misaada kutoka  nje, utawala  huo  unaendelea  kukataa misaada  hiyo  ya  kiutu.

Msemaji  wa  mpango  wa  chakula  wa  umoja  wa mataifa  amethibitisha  kuwa  shirika  hilo  limesitisha safari  zote  za  anga  za  kupeleka  misaada  nchini Burma wakati  ikiendelea  na  majadiliano  na utawala  wa  nchi  hiyo  kuweza  kuruhusu  misaada kuingia  nchini  humo.Kamishna  wa  misaada  ya maendeleo  wa  umoja  wa  Ulaya Louis  Michel amesema  leo  kuwa  hatua  hiyo ya  Burma haikubaliki  kabisa.

Katika  taarifa  leo  Ijumaa  wizara  ya  mambo  ya kigeni  ya  Burma  imesema  kuwa  haiko  katika nafasi  ya  kupokea  wafanyakazi  wa  mashirika  ya kigeni  ya  kutoa  misaada , ikisema  kuwa inashughulikia  mzozo  huo  kwa  uwezo  wake binafsi.

Wakati  huo  huo  kansela  wa  Ujerumani  Angela Merkel  ameliambia  shirika  la  habari  la  Ujerumani kuwa  nchi  hiyo  itajiunga  na  Ufaransa  katika kumtaka  katibu  mkuu  wa  umoja  wa  mataifa Ban Ki-moon  kuitisha  mkutano  wa  baraza  la  usalama la  umoja  wa  mataifa  kuhusu  mzozo  huo.