1. main content
  2. main navigation
  3. extra content
  4. head navigation
  5. search
  6. Choose form 30 Languages



 

News | 09.05.2008 | 14:00 UTC

Mbeki kuwa na mazungumzo na viongozi wa Zimbabwe.

Harare.


Mpatanishi  mkuu  katika  mzozo  wa  Zimbabwe rais  Thabo  Mbeki  wa   Afrika  kusini , amewasili  leo mjini  Harare  kwa  mazungumzo  na  rais  Robert Mugabe  kwa  ziara  yake  ya  kwanza  tangu kutangazwa  rasmi  matokeo  ya  uchaguzi  mkuu  wa rais.

Mbeki  ambaye  anakosolewa  kwa  kuchukua msimamo  laini   dhidi  ya rais  Robert  Mugabe, anatarajiwa  kukutana  na  kiongozi  huyo  mkongwe wa  Zimbabwe, lakini  haijafahamika   iwapo atakutana  pia  na  upande  wa  upinzani.Kiongozi wa  chama  cha  MDC  Morgan Tsvangirai  hivi  sasa yuko  nje  ya  nchi  hiyo  akikutana  na  viongozi  wa Afrika   pamoja  na  wanadiplomasia   katika  juhudi za  kuongeza  mbinyo dhidi  ya   Mugabe  mwenye umri  wa  miaka  84  kujiuzulu  baada  ya  miaka  28 ya  utawala  wake.

Chama  cha  MDC  pia  kimesema  kuwa  hakipangi kushiriki  katika  uchaguzi  wa  duru  ya  pili. Tsvangirai  hajatoa jibu  kamili  iwapo  atashiriki katika  uchaguzi  huo na  iwapo  hatatoa  jibu  kamili Mugabe  mwenye  umri  wa  miaka  84  atakuwa mshindi  moja  kwa  moja.

Pia chama  cha  MDC  kimesema  kuwa  hadi  sasa hakijapata  mwaliko kutoka  kwa  Mbeki  kukutana  na uongozi  wake  katika  ziara  yake  ya  siku  moja mjini  Harare.