1. main content
  2. main navigation
  3. extra content
  4. head navigation
  5. search
  6. Choose form 30 Languages



 

 | 16.05.2008 | 15:00 UTC

Bush - Israel yaweza kuitegemea Marekani.

Jerusalem.


Rais  Bush  wa  Marekani  ameliambia  bunge  la Israel  kuwa  Marekani  itasimama  pamoja  na  Israel katika  kuipinga  Iran  iwapo itajaribu  kujipatia  silaha za  kinuklia.

Bush  ameongeza  kuwa  anakichukulia  kwa umuhimu  wa  juu  kitisho kilichotolewa  na   rais  wa Iran  Mahmoud  Ahmedinejad  kuifuta  Israel  kutoka katika  ramani  ya  dunia. Akizungumza  umuhimu wa  kuitetea  Israel  katika  mashariki  ya  kati  Bush amesema.


O-Ton  Bush


Iran  imesema   kuwa  mpango  wake  wa  kinuklia una  lenga  katika  matumizi  ya  umeme.

Bush,  ambaye  yuko  katika  ziara  kuadhimisha kuasisiwa  kwa  taifa  la  Israel  miaka  60  iliyopita, ameliambia  bunge  la  Israel , Knesset  kuwa  Israel pia  inaweza  kutegemea uhusiano  usiolegalega  na Marekani.

Rais  Bush  ameondoka  nchini  Israel  alielekea nchini  Saudi  Arabia  leo  kuanza  ziara   nchini humo , ambayo  itakuwa  ni  maadhimisho  ya  miaka 75 ya  uhusiano  baina  ya  Marekani  na  nchi  hiyo ya Kifalme.