1. main content
  2. main navigation
  3. extra content
  4. head navigation
  5. search
  6. Choose form 30 Languages



 

 | 16.05.2008 | 15:00 UTC

Bin Laden awashutumu viongozi wa mataifa ya magharibi kuhusu miaka 60 ya Israel

Dubai.


Kiongozi  wa   kundi  la  kigaidi  la  Al-Qaeda  Osama bin Laden  amewashambulia   viongozi  wa  mataifa ya  magharibi  kwa  kushiriki  katika  maadhimisho  ya miaka  60  ya  kuasisiwa  kwa  taifa  hilo  la  Kiyahudi.

Akizungumza  katika  ujumbe   wa  katika  radio  leo Ijumaa , bin Laden  ameapa  kuendeleza mapambano  dhidi  ya  taifa  hilo  la  Kiyahudi pamoja  na  washirika  wake  na  kwamba  Waislamu hawatasalim amri  hadi  pale  Palestina itakapokombolewa  kabisa.

Ujumbe  huo  leo  umekuja  wakati  rais  wa Marekani  George  W. Bush  anakamilisha  ziara yake  nchini  Israel  kuadhimisha  miaka  60  tangu kuasisiwa  kwa  taifa  hilo.

Bin Laden  amesema  katika  ujumbe  huo  kuwa mapambano  kwa  ajili  ya  Palestina  ni  jambo linalosukuma  vita  vya Al-Qaeda  dhidi  ya  mataifa ya  magharibi.