1. main content
  2. main navigation
  3. extra content
  4. head navigation
  5. search
  6. Choose form 30 Languages



 

 | 16.05.2008 | 15:00 UTC

Rais wa China aenda katika eneo la tetemeko.


Beijing.


Rais  wa  China  Hu Jintao amekwenda  katika  mji wa  Mianyang  katika  jimbo  la  Sichuan  kuona binafsi  maafa   yaliyotokea  siku  ya  Jumamosi baada  ya  tetemeko  la  ardhi  kutokea  katika  eneo hilo.

Vyombo  vya  habari  vya  serikali   vimeripoti  kuwa rais  Hu  ametoa  wito  wa  kuongezwa  juhudi  katika kile  alichokieleza  kuwa  ni  awamu  muhimu  ya operesheni  ya  uokozi.

Maafisa  sasa  wanasema ,   wanahofu   kuwa  idadi ya  watu  waliokufa  inaweza  kuwa  juu  zaidi  ya 50,000.

Hadi  sasa , kiasi  cha  watu  22,000  wamethibitishwa kuwa  wamefariki, lakini  watu  wengine  kwa  maelfu hawajulikani  waliko. Mji  wa  Mianyang  umekuwa kituo  cha  kupokea  watu  walionusurika wanaomiminika  kutoka  katika   maeneo yaliyoathirika  karibu  na  eneo  tetemeko  hilo lilipotokea  kilometa  100  upande  wa  magharibi.