1. main content
  2. main navigation
  3. extra content
  4. head navigation
  5. search
  6. Choose form 30 Languages



 

 | 16.05.2008 | 15:00 UTC

Kamishna wa umoja wa Ulaya wa misaada aenda Burma.


Rangoon.


Kamishna  wa  maendeleo   wa   umoja  wa  Ulaya ameutaka  utawala  wa  kijeshi  wa  Burma kuruhusu  wafanyakazi  wa  kutoa  misaada  kuingia nchini  humo  ili  kusaidia   wahanga  wa  kimbunga kilicholeta  maafa  makubwa.

Afisa  wa  umoja  wa  Ulaya   amesema   kuwa   Louis Michel  ametumia  mkutano  wake  na  maafisa  wa kijeshi  wa  utawala  wa  Burma  mjini  Rangoon kuutaka  utawala  huo  kutoa  visa kwa  wataalamu wa   kutoa  misaada  wa  umoja  wa  Ulaya   pamoja na  uhuru  wa  kusafiri  kwa  mashirika  ya  kutoa misaada  ya  umoja  wa  Ulaya.

Michel  ameomba  kufanya  mkutano  na   waziri mkuu  wa  Burma  pamoja  na  waziri  wa  mambo  ya kigeni, na  kuomba  ruhusa  ya  kutembelea  eneo lililoshambuliwa  na  kimbunga  hicho  la Irrawaddy, ambalo  liliathirika  sana   na   kimbunga  Nargis karibu  wiki  mbili  zilizopita.

Mashirika  ya  kimataifa  ya  kutoa  misaada yamesema   kuwa  wahanga  milioni  2.5   wa kimbunga  hicho  wanahitaji  msaada   wa  haraka. Idadi  rasmi  ya  watu  waliokufa  hadi  sasa  imefikia 43,000, lakini  mashirika   ya  kimataifa  yanasema kuwa  idadi  halisi  inaweza  kuwa  zaidi  ya  watu 100,000.