1. main content
  2. main navigation
  3. extra content
  4. head navigation
  5. search
  6. Choose form 30 Languages



 

 | 16.05.2008 | 15:00 UTC

Mzozo wa Chavez na Merkel wagubika mkutano wa L.America.


Lima.


Kansela  wa  Ujerumani  Angela  Merkel  ameahidi msaada  kutoka  Ujerumani  kwa  ajili  ya  wizara  ya mazingira  nchini  Peru  wakati  wa  mkutano  na  rais wa  nchi  hiyo, Alan Garcia.

Kufuatia  mazungumzo  ya  viongozi  hao  wawili, Garcia  ameeleza  kumuunga  kwake  mkono  Merkel katika  mvutano  wake  wa  hivi  karibuni  na  rais  wa Venezuela  Hugo  Chavez.

Merkel  anatarajiwa  kukutana   na  Chavez , kandoni mwa  mkutano   wa  umoja  wa  Ulaya   na  mataifa ya  Latin  Amerika  unaofanyika  leo  Ijumaa  katika mji  mkuu  wa  Peru  , Lima.

Mkutano  huo  unatarajiwa  kujadili  umasikini  na mabadiliko  ya  hali  ya  hewa, lakini  umegubikwa  na mzozo  kati  ya  viongozi  hao  wa  Ujerumani  na Venezuela. Merkel  amezitaka  nchi  za  eneo  hilo kujiweka  mbali  na  serikali  ya  kisishalist  ya Venezuela, wakati  Chavez  amemshutumu  Merkel kwa   kuwa  katika  utamaduni  ule ule  wa  kisiasa wa   enzi  za  Nazi.