| 16.05.2008 | 15:00 UTC
uchaguzi wa duru ya pili Zimbabwe Juni 27
Harare.
Tume ya uchaguzi nchini Zimbabwe imesema leo kuwa uchaguzi wa rais wa duru ya pili utafanyika Juni 27.
Kiongozi wa upinzani Morgan Tsvangirai anatarajiwa kurejea nchini Zimbabwe kesho Jumamosi baada ya kuwapo nje ya nchi hiyo kwa muda wa zaidi ya mwezi mmoja kufuatia uchaguzi unaobishaniwa.
Tsvangirai ambaye hivi sasa yuko nchini Ireland ya kaskazini, anatarajiwa kurejea nchini humo na atawasili mjini Harare mchana, kwa mujibu wa mkurugenzi wa habari wa chama cha MDC Luke Tamborinyoka.
Baada ya uchaguzi wa March 29 kumekuwa na ghasia ambapo chama cha upinzani cha MDC , kinalaumu wanajeshi wa utawala utawala wa Zimbabwe.
Chama cha upinzani kinasema wanachama wake 40 wameuwawa na zaidi ya nyumba 1,000 zimeharibiwa ama kuvunjwa.
Chama cha ZANU -PF cha rais Robert Mugabe kimekanusha kuhusika na kukilaumu chama cha MDC kwa kuanzisha ghasia katika juhudi za kulichafua jina la rais Mugabe.






