1. main content
  2. main navigation
  3. extra content
  4. head navigation
  5. search
  6. Choose form 30 Languages



 

 | 16.05.2008 | 15:00 UTC

uchaguzi wa duru ya pili Zimbabwe Juni 27

Harare.


Tume  ya  uchaguzi  nchini   Zimbabwe   imesema leo  kuwa  uchaguzi  wa  rais  wa  duru  ya  pili utafanyika  Juni  27.

Kiongozi  wa  upinzani  Morgan  Tsvangirai anatarajiwa   kurejea  nchini  Zimbabwe kesho Jumamosi baada  ya   kuwapo  nje  ya  nchi  hiyo kwa  muda  wa  zaidi  ya  mwezi  mmoja  kufuatia uchaguzi  unaobishaniwa.

Tsvangirai  ambaye  hivi  sasa  yuko  nchini  Ireland ya  kaskazini, anatarajiwa  kurejea  nchini  humo  na atawasili  mjini  Harare  mchana, kwa  mujibu  wa mkurugenzi  wa  habari wa  chama  cha  MDC  Luke Tamborinyoka.

Baada  ya  uchaguzi  wa  March  29  kumekuwa  na ghasia  ambapo  chama  cha  upinzani  cha  MDC , kinalaumu  wanajeshi  wa  utawala   utawala  wa Zimbabwe.

Chama  cha  upinzani  kinasema  wanachama  wake 40  wameuwawa  na  zaidi  ya  nyumba   1,000 zimeharibiwa  ama  kuvunjwa.

Chama  cha  ZANU -PF  cha  rais  Robert  Mugabe kimekanusha  kuhusika  na  kukilaumu  chama  cha MDC kwa  kuanzisha  ghasia  katika  juhudi  za kulichafua  jina  la  rais  Mugabe.