1. main content
  2. main navigation
  3. extra content
  4. head navigation
  5. search
  6. Choose form 30 Languages



 

 | 16.05.2008 | 15:00 UTC

Umoja wa mataifa kurejea Somalia.

New York.


Baraza  la  usalama  la  umoja  wa  mataifa limepitisha  azimio  ambalo  linaweza  kufungua   njia kuwekwa  kwa   wanajeshi  wa  umoja  wa  mataifa wa  kulinda  amani  nchini  Somalia.

Licha  ya  kuwa  maandishi  ya   azimio  hilo  hayatoa ahadi  ya  kuwekwa  kwa  jeshi  la  umoja  wa mataifa, lakini  linatoa  wito  kwa  umoja  wa  mataifa kupanga  kuchukua  jukumu  la  ujumbe  wa kulinda  amani  ambao  kwa  sasa  unaendeshwa  na umoja  wa  Afrika.

Pia  azimio  hilo  linatoa  wito  kwa  taasisi  hiyo  ya dunia  kurejesha  operesheni  zake  za  kisiasa katika  nchi  hiyo  iliyoharibiwa  na  vita kutoka  nchi jirani  ya  Kenya. Serikali  ya  Somalia  inayoungwa mkono  na  Ethiopia, imekuwa  ikipambana   na wapiganaji  wa  Kiislamu  tangu  mwaka  2006.