| 16.05.2008 | 15:00 UTC
Umoja wa mataifa kurejea Somalia.
New York.
Baraza la usalama la umoja wa mataifa limepitisha azimio ambalo linaweza kufungua njia kuwekwa kwa wanajeshi wa umoja wa mataifa wa kulinda amani nchini Somalia.
Licha ya kuwa maandishi ya azimio hilo hayatoa ahadi ya kuwekwa kwa jeshi la umoja wa mataifa, lakini linatoa wito kwa umoja wa mataifa kupanga kuchukua jukumu la ujumbe wa kulinda amani ambao kwa sasa unaendeshwa na umoja wa Afrika.
Pia azimio hilo linatoa wito kwa taasisi hiyo ya dunia kurejesha operesheni zake za kisiasa katika nchi hiyo iliyoharibiwa na vita kutoka nchi jirani ya Kenya. Serikali ya Somalia inayoungwa mkono na Ethiopia, imekuwa ikipambana na wapiganaji wa Kiislamu tangu mwaka 2006.






