| 16.05.2008 | 15:00 UTC
Mkutano wa mataifa ya Ulaya na latin Amerika waanza.
Lima.
Viongozi kutoka mataifa 50 ya Ulaya , Amerika ya kusini na Caribik, wanakutana mjini Lima , Peru kujadiliana kuhusu umasikini, mabadiliko ya hali ya hewa na kuongezeka kwa bei za vyakula duniani. mkutano huo huenda ukashindwa kufikia makubaliano juu ya majadiliano ya kibiashara.
Tayari kikao hicho cha leo na kesho kimefunguliwa kwa mabishano miongoni mwa viongozi wa eneo hilo kuhusiana na biashara huria.
Halikadhalika malumbano kati ya rais Hugo Chavez na kansela wa Ujerumani Angela Merkel.Mwenyeji wa mkutano huo rais Alan Garcia wa Peru, amesema viongozi pia watajadiliana juu ya hali za kibinadamu.
Ameongeza kuwa masuala yatakayozingatiwa ni pamoja na hali za binadamu katika maendeleo ya teknolojia, utajiri na demokrasia pamoja na hali bora za kiutu.Rais Garcia pia amemtetea kansela wa Ujerumani Angela Merkel katika malumbano yake na kiongozi wa Venezuela Hugo Chavez.
O-Ton Garcia.
Hata hivyo kansela wa Ujerumani amesema kuwa anataka kuimarisha ushirikiano wa kimkakati na eneo hilo na pia kuwa na masikilizano na Chavez katika kikao cha leo kitakachofanyika pembezoni mwa mkutano huo.
Mivutano inayoongezeka kati ya viongozi wa eneo hilo la Amerika ya kusini inatishia kugubika makubaliano yoyote ya mwisho.






