1. main content
  2. main navigation
  3. extra content
  4. head navigation
  5. search
  6. Choose form 30 Languages



 

 | 16.05.2008 | 15:00 UTC

Mkutano wa mataifa ya Ulaya na latin Amerika waanza.

Lima.


Viongozi  kutoka  mataifa  50  ya  Ulaya , Amerika  ya kusini  na  Caribik, wanakutana   mjini  Lima , Peru kujadiliana  kuhusu umasikini, mabadiliko  ya  hali  ya hewa   na  kuongezeka  kwa  bei  za  vyakula duniani. mkutano  huo  huenda  ukashindwa  kufikia makubaliano  juu  ya  majadiliano  ya  kibiashara.

Tayari  kikao  hicho  cha  leo na  kesho kimefunguliwa  kwa  mabishano  miongoni  mwa viongozi  wa  eneo  hilo  kuhusiana  na  biashara huria.

Halikadhalika  malumbano  kati  ya  rais  Hugo Chavez  na  kansela  wa  Ujerumani  Angela Merkel.Mwenyeji  wa  mkutano  huo  rais  Alan Garcia wa  Peru, amesema  viongozi  pia  watajadiliana  juu ya  hali  za   kibinadamu.

Ameongeza   kuwa  masuala  yatakayozingatiwa  ni pamoja  na  hali  za  binadamu  katika  maendeleo ya  teknolojia, utajiri  na  demokrasia  pamoja  na hali  bora  za  kiutu.Rais  Garcia  pia  amemtetea kansela  wa  Ujerumani  Angela  Merkel  katika malumbano  yake  na  kiongozi  wa  Venezuela Hugo Chavez.


O-Ton  Garcia.


Hata  hivyo kansela  wa  Ujerumani  amesema  kuwa anataka  kuimarisha  ushirikiano  wa  kimkakati  na eneo  hilo  na  pia  kuwa  na  masikilizano  na Chavez  katika  kikao  cha  leo  kitakachofanyika pembezoni  mwa  mkutano  huo.

Mivutano  inayoongezeka  kati  ya  viongozi  wa  eneo hilo  la  Amerika  ya  kusini  inatishia  kugubika makubaliano  yoyote  ya  mwisho.