1. main content
  2. main navigation
  3. extra content
  4. head navigation
  5. search
  6. Choose form 30 Languages



 

 | 16.05.2008 | 15:00 UTC

dalai Lama atoa wito wa kujitawala zaidi Tibet

Bochum, Ujerumani.


Kiongozi  wa  kidini  wa  Tibet  Dalai  lama anaendelea  na  ziara  yake  ya  siku  tano  nchini Ujerumani  akiwa  katika  mji  wa  Bochum.

Kiongozi  huyo  wa  kidini  amewashukuru  waungaji wake  mkono  katika  bara  la  Ulaya  wakati  kwa mara  nyingine  tena  amesisitiza   kuwa  anatafuta kujitawala  zaidi  kwa  jimbo  lake  la  Tibet, na  sio uhuru  kamili.

Jana  Alhamis  Dalai  Lama  alikutana  na  viongozi wa  kisiasa  wa  eneo  la  Ulaya   pamoja  na   rais wa  bunge  la  Ujerumani, Nobert  Lammert.

China  tayari  imepinga   mipango  ya  kukutana  siku ya  Jumatatu  na  waziri  wa  maendeleo  wa Ujerumani  Heidemarie Wieczorek-Zeul.

Mwaka  jana  kansela  Angela  Merkel  alikutana  na Dalai  Lama  mjini  Berlin,  hatua  ambayo ilisababisha  uhusiano  kati  ya  China  na  Ujerumani kuingia  dosari.